Saturday, September 3, 2016

Polisi: Wanafunzi muwe tayari kutoa ushahidi katika vyombo vya sheria



Wanafunzi nchini wametakiwa kujikita zaidi katika masomo yao na kujiepusha kujiingiza katika makundi hatarishi yanayoweza kuwapelekea kujihusisha na matumizi ya maadwaya ya kulevya.

Akitoa elimu ya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanafunzi wa skuli ya Sekondari BUBUBU msaidizi mkaguzi kitengo cha upepelezi kituo cha polisi Bububu   Jongo Ali Jongo amesema kujiingiza kwa  matumizi  ya madawa ya kulevya yataweza kuwapelekea kujihusisha na vitendo vya udhalilishaji.
Nae Koplo Khamis Muhammed Rashid wa kitengo cha upelelezi  Bububu amewataka wanafunzi kuwa tayari kuvifichua vitendo vyote vya udhalilishaji wa kijinsia kwa kuwa tayari kutoa ushahidi katika vyombo vya sheria.
Na;Fat hiya sheheZanzibar24
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © TODAY'S YOUTH FOUNDATION | Designed by Francis Ikomba Distributed By Norbert Inc.