Tuesday, September 26, 2017

Monday, September 25, 2017

Tundu Lissu Amtumia Salamu Waziri Ummy Mwalimu...Adai Atamjibu Mwenyewe


RAIS wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu,  ameibuka na kusema, “vijembe vinavyorushwa na Ummy Mwalimu,” Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, “vitajibiwa na mimi mwenyewe,”

Akihutubia mkutano wa nusu mwaka wa mawakili nchini (AGM), kaka mkubwa wa Lissu, Alute Mughwai Lissu, ameeleza kuwa ameelekezwa na mdogo wake huyo, kutomjibu Ummy Mwalimu, badala yake kazi hiyo itafanywa na yeye mwenyewe.

Alute ambaye ni wakili wa kujitegemea anayefanya shughuli zake mkoani Arusha ameuambia mkutano huo, “nimeongea na Lissu leo saa nne asubuhi. Amenielekeza kuwa familia isijibu hoja za waziri Ummy Mwalimu.”

Amesema, “kazi hiyo itafanywa na yeye mwenyewe mara akataporejea nchini kutoka kwenye matibabu yake nje ya nchi. Ameahidi kuendeleza mapambano ya kudai haki bila kuchoka.”

Wakili Alute amesema, Lissu amemueleza kuwa “hatarudi nyuma katika harakati zake za kutetea haki na demokrasia nchini. Ameapa kupambana hadi tone lake la mwisho.”

Kwa mujibu wa Alute, afya ya Lissu inaendelea vizuri na anawashukuru madaktari wanaomtibu kwenye hospitali ya Nairobi alikolazwa. Amewataka wajumbe wa mkutano huo kuendelea kumuombea.

Alute alikuwa akitoa salamu kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa TLS uliofanyika jana mjini Arusha.

Hii ni mara ya kwanza kwa Lissu kuzungumza kwa simu tokea aliposhambuliwa kwa risasi na wanaoitwa na serikali, “watu wasiofahamika,” ambako alimiminiwa rundo la risasi zilizolenga kuondoa maisha yake.

Wakati huohuo, akiongea na Azam TV, Alute Lissu amesema kwamba familia yake imemwandikia barua Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakiomba uchunguzi wa tukio la kushambuliwa mdogo wake ufanywa na vyombo kutoka nje ya nchi, kwani katika mazingira ya sasa jeshi la polisi haliko tayari na haliko huru kufanya uchunguzi huo kwani hadi sasa hakuna mtu yeyote aliyekamatwa.

Kuhusiana na serikali kuitaka familia iandike barua ya kuomba matibabu kwa ajili ya Tundu Lissu, kaka yake huyo alisema mdogo wake huyo ambaye anatibiwa Nairobi amemwambia suala hilo atakuja kulizungumzia yeye akiwa ni mbunge mwenye haki zote za kupewa matibabu kama wabunge wengine.

Vyanzo: Mwanahalisi na Azam TV.
Share:

KESI YA MANJI KUUNGURUMA KISUTU LEO, MASHAHIDI WAKE KUTOA UTETEZI




Aliyekuwa Mwenyekiti wa Yanga, Yusuph Manji, leo Jumatatu anatarajiwa kuwapeleka mashahidi wake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa ajili ya kutoa utetezi wa kesi inayomkabili ya utumiaji wa madawa ya kulevya.

Manji anakabiliwa na kesi hiyo ambayo ilishindwa kusikilizwa Septemba 18, mwaka huu kufuatia wakili wa serikali, Timony Vitalis kumueleza Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha kuwa, kesi hiyo iliitishwa kwa ajili ya kuendelea na ushahidi lakini yeye alidai kuwa alikuwa na safari siku hiyo, hivyo ukianza kutolewa ushahidi atakuwa amechelewa.

Kutokana na wakili wa serikali kueleza hivyo, Hakimu Mkeha alimlaumu Manji kwa kuwa alichelewa kufika mahakamani hapo kabla ya kuomba msamaha huku wakili wake Hajra Mungula akiomba Mahakama iwape kibali cha kupeleka mashahidi wao pamoja na kusikilizwa kwa mfululizo.


Hata hivyo, hakimu Mkeha alikubali maombi yao ya kusikilizwa kesi hiyo mfululizo kwa siku ya leo Jumatatu na kesho Jumanne katika mahakama hiyo.
Share:

Sunday, September 24, 2017

Serikali kuwabana wakala wa vyuo vikuu vya nje ya nchi


Tume ya Vyuo vikuu Tanzania (TCU), imesema tayari kuna sheria na wanadhibti wakala ama wawakilishi wa vyuo vikuu vya nje ya nchi wanakokwenda kusoma elimu ya juu vijana wa Kitanzania, ambapo kubwa ni sifa za kusoma vyuo hivyo iwe sawa na ya kusoma vyuo vya nchini.

Afisa habari mwandamizi wa TCU, EDWARD MKAKU, ameyasema hayo wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wanafunzi zaidi ya 200 wanaotarajiwa kuondoka nchini Septemba 27 mwaka huu, kwenda Marekani, Ulaya, Asia na Afrika Kusini, katika vyuo vinavyowakilishwa hapa nchini na Universal Abroad Representatives (UAR), ambapo amewatoa hofu wazazi wa watoto husika, kuwa TCU, inawatambua wawakilishi hao.


Kwa upande wake TONY KABETHA, ambaye ni Mkurugenzi Mkuu Mkazi wa Taasisi hiyo inayoviwakilisha vyuo vya nchi za Marekani, Australia, China, Norway, Canada, Uingereza, Sweden, Denmark na India, amesema, wanafunzi hao wote shahada zao za kwanza zitajikita katika masuala ya teknolojia za viwanda pamoja na sekta ya mafuta na gesi, zinazotarajiwa kuwa chachu ya uchumi wa Tanzania.
Share:

Kwa sasa Cesar Azpillicueta na Alvaro Morata ndio combination hatari kuliko yoyote barani Ulaya


Hii leo mtaani mashabiki wa Chelsea wanatembea vifua mbele baada ya hapo jana Alvaro Morata kuionesha dunia ni nini amekuja kufanya Uingereza na kuwanyamazisha waliokuwa wanamsema.

Tayari Conte amemwagia sifa nyingi mshambuliaji huyo na kusema kwamba ni kijana mzuri sana kiasi kwamba hata kama una binti unataka muoezesha baasi muozeshe kwa Alvaro, lakini kuna mambo yafuatayo ya kufahamu kutokana na ushindi wa jana wa Chelsea.

Alvaro Morata alifunga hat trick yake ya kwanza, lakini je unajua ya kwamba hat trick hii ya Morata imechukua muda mrefu tofauti na Diego Costa. Diego Costa yeye alitumia mechi 4 tu kufunga hat trick huku Morata akitumia 6.

Wakati Morata akifanya hivyo, mchezaji mwingine mpya Chelsea Tiemoue Bakayoko yeye kwa siku ya jana alifanya tackle zilizofanikiwa 5, hiyo ni idadi ambayo jana katika michezo yote hakuna kiungo aliyemzida kwa tackling.

Chelsea hapo hapo, baada ya magoli matatu ya jana ya Morata inawafanya Chelsea kwa sasa mabao 10 kati ya 13 waliyofunga msimu huu yamefungwa na watu wa taifa moja la Hisapania.

Lakini vile vile kama hujui tu ni kwamba katika ligi 4 kubwa barani Ulaya hakuna Combination ambayo imezalisha mabao mengi hadi sasa kama combination ya Alvaro Morata na Cesar Azipiculeta, hadi sasa wametengeneza mabao manne.
Share:

Dreva wa Lissu Asema Hana Kumbukumbu Vizuri Kwa Kilichotokea Kwenye Shambulio Dhidi ya Lissu


Dereva wa Lissu ambaye ndiye mtu pekee waliyekuwa wote si ya tukio hilo, Simon Bakari naye alizungumza kwa mara ya kwanza kuhusu tukio hilo na kudokeza kwamba limevuruga na hana kumbukumbu sahihi.

Dereva huyo ambaye naye anaendelea kupatiwa matibabu ya kisaikolojia katika hospitali hiyo ya Nairobi alisisitiza, “Kwa sasa siwezi kuzungumza vizuri tukio hili kwani nadhani sina kumbukumbu vizuri.”

CHANZO GAZETI LA MWANANCHI
Share:

Saturday, September 23, 2017

Njia Rahisi Ya Kupata Mimba Haraka Kwa Mwanamke


  1. Kufanya tendo la ndoa mara kwa mara, angalau siku tatu kwa wiki, ikiwezekana on alternate days.
  2. Tumia ovulation prediction kit, hiki ni kifaa ambacho kitakusaidia kujua wakati hasa mwanamke ameengua yai na ndio kipindi ambacho mwanamke ana uwezo wa kushika mimba akikutana na mumewe. Ni rahisi kutumia.
  3. Fanya tendo la ndoa kabla ya kuengua yai (kabla ya ovulation), huongeza uwezekano wa kushika mimba kuliko kusubiria ovulation au kufanya baada ya ovulation. Kutaneni siku mbili au tatu kabla ya ovulation. Ukitumia ovulation test kit, mkutane kuanzia siku itakapokuwa positive kwani huwa inapredict ovulation kutokea 48 hrs after it tests positive.
  4. Usitegemee njia ya kalenda kutabiri uenguaji yai, njia hii kwa kiasi fulani huweza kuwasaidia wale wenye mzunguko wa siku 28, lakini pia haina uhakika wa 100%, wengi wa wanawake hawaengui yai siku ya 14 ya mzunguko wa hedhi, kwa hiyo kutegemea kalenda kutakuchelewesha kupata ujauzito.
  5. Unapotaka kushika mimba, acha au punguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya pombe, sigara au dawa za kulevya.
  6. Unapotaka kupata mimba, tendo la ndoa liwe kitu 'enjoyable' na sio tendo 'mechanical' kwa ajili ya kutafuta mtoto. Plan a romantic evening or try something different to spice things up. How you are feeling sexually may increase your chances of getting pregnancy. For women a better orgasm may help pull the sperms into the uterus and for men a better orgasm may increase their sperm count.
  7. Kufanya mapenzi katika mtindo (style) ambayo itafanya mbegu za kiume zikae kwa muda mrefu ukeni na hivyo nyingi kupanda kuingia kwenye kizazi na kwenda kurutubisha yai. 'missionary position' ni nzuri zaidi, ambapo mwanaume anakuwa juu, epuka positions za mwanamke kuwa juu kwani hufanya mbegu zimwagike kwa gravity. Jaribu pia kuweka mto chini ya kiuno ili kukiinua na kufanya mbegu ziingie ndani kwa urahisi zaidi.

Kumbuka kuna asilimia 10 - 25 ya couples ambazo zina matatizo ya infertility lakini vipimo havionyeshi tatizo, inaweza kuwa namna ya kufanya mapenzi ndio ikawa shida, jaribu njia hizo 7 juu.

Share:

Tuesday, September 5, 2017

Sunday, September 3, 2017

Copyright © TODAY'S YOUTH FOUNDATION | Designed by Francis Ikomba Distributed By Norbert Inc.