Monday, September 5, 2016

Vanessa Mdee atumbuiza na 2 Face kwenye show ya Buckwyld N Breathless, Lagos


Katika sehemu ambayo Vanessa Mdee ameshalikita jina lake vyema nje ya Tanzania, basi ni Nigeria.
 Muimbaji huyo wa ‘Niroge’ Jumamosi hii alikuwa mmoja wa waimbaji walioipamba show kubwa ya msanii mkongwe wa Nigeria, 2 Face Idibia iliyopewa jina, Buckwyld N Breathless. Show hiyo ilifanyika Eko Hotels & Suites, jijini Lagos.


Vee ambaye alitengeneza pair iliyovuma zaidi kwenye Coke Studio Afrika mwaka jana na 2 Face, hakuwa mchoyo wa fadhila kumshukuru muimbaji huyo kwa nafasi aliyompa.
“This picture describes everything I was feeling last night,” ameandika Vanessa kwenye picha akiwa na 2 Face jukwaani aliyoiweka Instagram.
“I thankyou @official2baba for constantly inspiring and elevating youngns like myself. I’m humbled and eternally gratefully.”

2 Face amewahi kukaririwa akimtaja Vanessa kuwa ni mmoja wa waimbaji anaowakubali Afrika.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 TODAY'S YOUTH FOUNDATION | Designed by Francis Ikomba Distributed By Norbert Inc.