Friday, April 14, 2017

Maamuzi Ya Kamati Ya Saa 72 Kuhusu Rufaa Ya Simba Kwa Kagera














Kamati ya saa 72 iliyokaa kikao leo April 13 na kuamua kuhusu malalamiko ya Simba kwaKagera Sugar kuhusu kumtumia mchezaji Mohamed Fakhi katika mchezo dhidi yao April 2 2017 akiwa na kadi tatu za njano kinyume na taratibu na kanuni za Ligi.

Simba walipeleka malalamiko hayo katika bodi ya Ligi na kuomba ipitie ripoti za waamuzi ili kujulikana ukweli, leo April 13 kamati ya saa 72 chini ya mwenyekiti wake Hamadi Yahayailikaa na kujiridhisha kuwa Kagera walikiuka taratibu hizo kwa mujibu wa Kanuni Simbawamepewa point zote tatu za mchezo dhidi yao.

Kamati imejiridhisha kuwa mchezaji Mohamed Fakhi alioneshwa kadi za njano katika mchezo dhidi ya Majimaji, Mbeya City na African Lyon, hivyo hakustahili kucheza katika mchezo dhidi ya Simba uliyochezwa April 2 2017 uwanja wa Kaitaba na Simba ikapoteza kwa magoli 2-1.


Share:

Copyright © TODAY'S YOUTH FOUNDATION | Designed by Francis Ikomba Distributed By Norbert Inc.