Friday, April 14, 2017

Rais Magufuli Amempigia Simu Mwana FA


Jioni ya April 12 2017 staa wa muziki wa hip hop bongo Hamisi Mwinjuma ambaye wengi tunamfahamu kwa jina la Mwana FA, alitoa taarifa kupitia ukurasa wake wa twitter kuoneshwa kufurahisha na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli kumpigia simu.
Mwana FA ambaye kwa sasa anafanya vizuri katika radio na tv stations mbambali kwa hit single yake ya Dume Suruali amethibitisha kupigiwa simu na Rais kumwambi anakubali kazi zake.

Kupitia ukurasa rasmi wa twitter wa staa huyo uliyokuwa verified aliandika “nimefurahi kupokea simu ya Mheshimiwa Rais @MagufuliJP kunisalimia na kuniambia yeye ni mpenzi wa kazi zangu,haswa #DumeSuruali..”
Share:

Copyright © TODAY'S YOUTH FOUNDATION | Designed by Francis Ikomba Distributed By Norbert Inc.